Popular Posts
-
Wife goes to supermarket, sees m e n's briefs on sale. She buys a dozen of the same colour. Goes home and gives hubby. Hubby protests...
-
Real Name : Haifa Mapili DOB : 27th Nov Lives at Sala Sala, DSM. Education : B.A (C.B.E) Songs out : PAYDAY and TATAKELE Up...
-
Mtoto wa kiume ni wa kiume tuu... tangu utoto utaona tabia zake. sasa hapo kwenye sanamu la dukani anachungulia nini?????
-
Silly Larry........... Larry alipochoka kufanya kazi zake akazima taa, akambusu mkewe, akalala na usingizi mzito ukampitia. Mara ak...
-
kama wewe ni mzazi au mlezi basi yakubali majukumu yako na uyazingatie... si haki na haipendezi kumbambika mtoto mdogo kiasi hichi majukumu ...
-
wapo watu, sijui ni kwa nini hasa. Lakini wakimaliza haja zao hawaoshi mikono! Wengi ni akina baba... sasa haya masinki ni kiboko yao. Hapo ...
-
Sales lady: Sorry sir u can't smoke here. Man: But I bought the cigarette in this shop. Sales lady:...
Sunday, September 23, 2012
Friday, September 21, 2012
2nite @ Rudy's Farm...
The sexy & unique Bar at Rudy's
farm, made of brick work burned
RED, reclaimed dhow wood and
recycled metal....
Twist the yard - with deejay
handsolo on the mix - tonight!
Njooni WOTE!
Thursday, September 20, 2012
Wednesday, September 12, 2012
Today's joke...
Jamaa alienda kuposa kwa mzee mmoja.
Mzee:Umekuja kuposa huku unatafuna bigji!?
Jamaa:Natoa harufu ya sigara.
Mzee:Yani unavuta sigara!?
Jamaa:Vile nikitoka kilabu kulewa tu huwa napenda kutumia sigara.
Mzee:Unalewa!?
Jamaa:Nilianza kulewa nilipokuwa jela.
Mzee:Yaani na kufungwa pia!?
Jamaa:Ah niliua mtu.
Mzee:/uh kumbe wewe muuaji!?
Jamaa:Ah,si kuna mzee nilitaka kumposa mwanae akanikatalia,mimi nikamuulia
mbali.
Mzee:Karibu baba, unataka harusi lini? Mimi sina tabu, Mkeo huyooo.!
Monday, September 10, 2012
Vijana na mahusiano...
Na Ikunda Faustine, Dar...
Nilikuwa namsikiliza Bi Ponza juzi anasema wasichana wa sasa
hawajui kupika kabisa.Wengi wanaendekeza urembo sanaaa, vi-picha picha, vi-facebook nk. lakini kupika hawajui, Je ni
kweli?
Nimekuwa nikisikia ili umkamate mwanaume pamoja na mautundu
mengine uwe unajua kumpikia mahanjumati.Hivi ni kweli katika maisha tuliyopo
wanaume wanajali sana kuhusu mapishi au mwanamke anaempikia madikodiko? TAFAKARI...
KWA WANAUME NAO:- MAMBO 6 WANAUME WASIYOYAPENDA KUTOKA WA
WENZA WAO.
1. Wanaume hawapendi kuambiwa cha kufanya na wenzi wao
Mwanamke unapotaka mwanaume afanye jambo usimwambie alifanye
bali fanya kama una mpa ushauri.Kwamba John hivi kwa nini tusiweke balbu hapa
kwenye korido maana kuna giza kweli usiku. Badala ya hivi "wewe John huoni hapa kwenye
korido kuna giza balbu imeungua mwezi sasa hujabadilisha kwa nini? Weka balbu
bwana". Atafanya au asifanye kabisa kwa sababu umemwambia cha kufanya tena kwa hasira.
2. Wanaume hawapendi mwenzi mwenye makelele, mlalamishi
Yeye ni kulalamika kuanzia jumatatu hadi jumapili. Japo wanawake
nao wanasema kuna wanaume walalamishii balaaa. Na wenye gubu wanasusa kula mpaka
kuongea wanawanunia wake zao mmmmh!
3. Wanaume hawapendi mwenzi mchafu
Mchafu wa mwili wake na hata nyumbani kwenye suala la
kutunza nyumba wanayoishi. Uchafu hufanya mwanamke apoteze mvuto.
4. Wanaume hawapendi mwenzi mbishi
Japo na wanawake wanasema wanaume ndio wabishi zaidi. Utampa
mwanaume ushauri lakini haufanyii kazi ubishi mwingi mpaka kwenye mambo ya msingi.
5. Wanaume hawapendi kuamrishwa na mwenzi wao
Mwenzi mbabe anaetoa amri na kumtawala hawataki.
6. Wanaume hawapendi kuhisiwa hisiwa na kusachiwa sachiwa
Kumpekua kwenye simu, mifuko ya suruali kwamba unamulika
mwizi. Hawapendi, tena pengine hawajafanya jambo la kuwafanya wahisiwe vibaya.
Friday, September 7, 2012
Sunday, September 2, 2012
Saturday, September 1, 2012
Subscribe to:
Posts (Atom)


















