Tanzania ya leo ni tofauti kabisa na Tanzania ya miaka ya nyuma, hasa kwa
Dar-es-salaam. Mwanamke kulala na mwanaume imekuwa ni kitu cha kawaida sana,
sio kama zamani. Zamani mwanamke kulala nae sio kazi ndogo. Utaambiwa subiri
nikafikirie, jibu wiki ijayoooooo! Pengine tungesema tatizo kwa sasa ni low
self esteem na low self confidence kwa kina dada, lakini hata huko vyuoni nako
ambako tunategemea kina dada zetu wasomi wawe tofauti, wao ndio wamepitiliza
kabisa. Hao ndio wanao ongoza kwa mambo yote ya aibu mjini DSM. Makazini ndio
usiseme, ni kawaida kwenda chooni na kusikia mke wa mtu anapiga mayowe ya
mahaba. Kwa kweli tofauti na zamani, suala la sex halina thamani tena. Kwenye
ndoa ndio kabisa, ni jambo la kawaida kwa wake za watu kulala na vidume vyao
vya zamani, hata kama huko walipoolewa kuna kila juhudi za kuwaridhisha. Swali
langu ni je, hali hii ya ngono ya ovyo ovyo na rahisi rahisi ni nani wa
kulaumiwa zaidi kati ya wanaume na wanawake? Kwani humu kumekuwa na thread
nyingi sana za kulaumu wanawake hawajatulia, mara nyingine wanaume hawajatulia,
lakini huwa hakuna mjadala wa kusaidiana kupata majibu kuhusu chanzo la tatizo
hili, hasa kwa kuzingatia kwamba huko nyuma hali haikuwa hivi.
Popular Posts
-
Miss Tanzania wa kwanza akipita ukumbini kweye bwalo la kuogelea ndani ya Kilimanjaro Hotel Mwaka 1967. Anaitwa Theresia Shayo. Urembo b...
-
Dr. Banda also claimed substantial parts of Tanzania, including - Rungwe district - and the rest of Mbeya Region in southwestern Tan...
-
Raisi wa Nigeria Umaru Yar'Adua (pichani) amefariki dunia siku ya Jumatano mwezi wa tano akiwa na miaka 58. Marehemu Yar'Adua ali...
-
THESE amazing pictures show the moment Swaziland’s former Justice Minister Ndumiso Mamba was caught by state security agents holed up in ...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment